Wednesday, December 5, 2012

Mstari wa Leo

Yeremia 33:3 “Niite nami nitakuitikia, nami nitakuonyesha mambo makubwa, magumu usiyoyajua”
 
Pengine kila mtu anaweza shuhudia ni mstari gani wa Biblia umembariki. Kipekee mstari huu unanibariki sana. Sina budi kusema Mungu ameniitikia nilipomuita na anaendelea kunionyesha mambo mengi ambayo kwa akili zangu nisingeweza kuyafikia. Usichoke kumuomba Mungu na kulisoma neno lake. Wapo baadhi ya watu ambao wanaamini wakitaka kumuona Mungu lazima waongee na watumishi fulani yaani wawe wanapewa maono. Kutaka kumuona Mungu sio lazima umtafute mtumishi fulani akuonyeshe. Mungu yupo kwako kila dakika na kila saa. Muite yeye yu karibu na husikia kila tumuitapo.
Ubarikiwe!

 

No comments:

Post a Comment