Wednesday, August 14, 2013

Neno la Leo



Efe 5:33 “Lakini kila mtu ampende mke wake kama nafsi yake mwenyewe; wala mke asikose kumstahi mumewe”

TAFAKARI: Ndoa ni zawadi ya muhimu na inatoka kwa Mungu. Tumuombe Mungu aziangalie na kuzilinda ndoa zetu. Na zaidi atusaidie kuheshimu maamuzi ya kila mmoja wetu katika ndoa (Mme na mke).

SALA: Mwenyezi Mungu nasema asante kwa kunipa mme mzuri. Naomba umuongoze katika kunipenda na kunijali tunapofanya kazi pamoja kwa ajili ya maisha yetu ya baadae. Bwana, naomba kwamba siku zote tutegemee muongozo wako, na zaidi tufwate mfano wa upendo wako usio na kifani. Tunaomba utuonyeshe njia ambazo tunaweza kuinuana wenyewe kwa wenyewe hasa pale tunapokutumia wewe. Katika jina la Yesu naomba na kupokea, Amen.

1 comment: