Tuesday, July 30, 2013

Neno la leo



Yoh 14: 6-7 “Yesu akamwambia, Mimi ndimi njia na kweli na uzima; mtu haji kwa Baba, ila kwa njia ya mimi. Kama mngalinijua mimi, mngalimjua na Baba; tangu sasa mnamjua, tena mmemwona”

TAFAKARI: Ni baraka kubwa kuweza kumuona Mungu. Kwa  kusoma neno lake tunapata picha ya sifa zake, uhalisia wake na upendo wake.

SALA: Mwenyezi Mungu, kila siku najitahidi kumjua Yesu Kristo kwa sababu natambua yeye ataniweka karibu nawe zaidi. Atanisogeza karibu na ukweli wa uumbaji wako na ukamilifu wako. Nimekuwa na nguvu kuliko kawaida kwa sababu nafwata hii kiu ya kukuelewa wewe na mwanao Yesu, Kristo. Naomba mapenzi yako yatimie katika haya yote, Amen.

No comments:

Post a Comment