Friday, January 4, 2013

Heri ya Mwaka Mpya!

Zab 5:1 “Ee Bwana, uyasikilize maneno yangu, ukuangalie kutafakari kwangu”

TAFAKARI: Mungu wetu husikiliza tumuitapo na kutuwezesha kufanya maamuzi katika mambo yetu pale tumshirikishapo.
SALA: Mwenyezi Mungu nasema asante kwa maana umeniwezesha kuuona mwaka huu mpya. Bwana naomba unisaidie katika kuutafakari mwaka huu na uniongoze kuyafikia yale niliyoazimia kwa mwaka huu.Zaidi nizidishie maarifa, busara na hekima ili niweze kuishi vyema na jamii inizungukayo. Katika jina la Yesu naomba na kushukuru, Amen.

 

 

No comments:

Post a Comment