Thursday, October 18, 2012

NENO LA LEO


“Ndugu sijidhanii nafsi yangu kwamba nimekwisha kushika ila natenda neno moja tu nikiyasahau yaliyo nyuma, nikiyachumilia yaliyo mbele” Wafilipi 3:13

Pengine unajiskia mnyonge na kujilaumu kutokana na mambo uliyoyafanya wakati uliopita na vile vile haupo pale ambapo Mungu anataka uwepo. Mungu anajua kila chaguo baya la mtu, anajua magumu unayopitia, kila baya ulilotenda na hakika amekuandalia mpango wa kukurudisha kwake. Usikate tamaa kwa maana kushindwa sio mwisho wa kila kitu, Mungu pekee ndiyo mwenye kuamua katika mambo yote. Makosa uliyoyafanya yasiwe sababu ya kukukosesha kuwa karibu na Mungu. Pengine leo hii uko kwenye uhusiano ambao huoni mwanga mbele yako ama una matatizo ya kifedha na magonjwa yanakuandama, Mungu pekee ndiye atakayekuokoa. Endelea kumtumaini na kumwamini yeye hakika atakuinua na kukupitisha kwenye vizingiti ambavyo hukudhani kama utaweza kupita. Mungu amemuandalia kila mtu destination yake, so never lose hope.
I love this song, such moving words it carries!
 

No comments:

Post a Comment