Monday, October 13, 2014

Neno la leo

Wafilipi 2:12 “Basi, wapendwa wangu kama vile mlivyotii sikuzote si wakati mimi nilipokuwa tu, bali sasa zaidi sana mimi nisipokuwapo, utimizeni wokovu wenu wenyewe kwa kuogopa na kutetemeka”

TAFAKARI: Maandiko matakatifu yanatuasa kuutimiza wokovu wetu kwa kuogopa na kutetemeka. Tudumu katika neno lake na kuzitii amri zake ili tuweze kusimama imara katika imani yetu ya wokovu. Na zaidi tuepuke kulitumia neno la wokovu kwa kuficha mambo yetu mabaya. Katika kufanya haya yatupasa kujitwika msalaba wake na kuwa mfuasi wake na kufanya yale yampendezayo. Vile vile kutambua eneo lako kama mkristo ni lipi ambalo litakufanya utimize wokovu wako.


SALA: Bwana Yesu, tunakuja mbele zako kwa unyeyekevu kabisa tukiomba utujalie maskio ya kuskia na kudumu katika neno lako. Tuwezeshe kuutambua wokovu wetu na kuushika tusiterereke kamwe. Zaidi tusaidie kuwa mfano wa wafuasi wako tukiubeba msalaba wako kwa imani na ya kwamba ipo siku tutafurahia matunda ya wokovu wetu. Tunaomba hayo na kupokea, Amen.

No comments:

Post a Comment