Monday, July 1, 2013

Neno la leo


Zab 119: 30 “Nimeichagua njia ya uaminifu, Na kuziweka hukumu zako mbele yangu”

TAFAKARI: Sio njia zote huwa zinapitika kwa maana nyingine zina miba ama vitu vingine vya hatari ambapo si rahisi kwa mwanadamu kupita. Hivyo basi, tumuombe Mungu atuonyeshe njia zile ambazo tunapaswa kupita.

SALA: Nashukuru sana nimegundua ukweli kwa wakati muafaka, kwa maana nilikuwa kila mahali na maswali ya hapa na pale. Bwana, wakati mwingine sikujua niulize maswali gani ili tu nikate kiu yangu ya kuelewa na kujitambua. Asante kwa kuwa umenitoa kwenye ujinga na kunionyesha nuru ya moyo wako, na hapo mambo yangu yalianza kwenda kama wewe ulivyopendezwa. Naomba uzidi kunionyesha njia Mungu wangu ili niingie kwenye mitego ya muovu shetani. Naomba hayo na kupokea katika jina la mwanao Yesu Kristo, Amen.

No comments:

Post a Comment