Monday, June 24, 2013

Neno la Leo


Mat 21:22 “Na yoyote mtakayoyaomba katika sala mkiamini, mtapokea”

TAFAKARI: Jambo la muhimu la kujiuliza hapa ni kwamba unaamini? Unaamini ya kwamba Bwana Mungu yupo na pindi tumuombapo kitu chochote hutupatia?

SALA: Bwana nakiri ya kwamba naamini uwepo wako na ninajua ya kuwa nikiomba unanijibu sawasawa na mapenzi yako. Hata pale ambapo ninatambulika kwa kukosa kujiamini, ninachoomba kutoka kwako ni muongozo, busara na amani katika mambo nifanyayo. Unaniongezea Imani Bwana, pale unapojibu sala zangu. Naomba mkono wako wa busara na hekima usinipungukie ninapoendelea kukutumaini wewe katika maisha yangu. Katika jina la Yesu Kristo naomba na kupokea, Amen.

No comments:

Post a Comment