Tuesday, December 18, 2012

Neno la leo

“Kila mtu na atende kama alivyokusudia moyoni mwake, si kwa huzuni wala si kwa lazima, maana Mungu humpenda yeye atoaye kwa moyo wa ukunjufu,” 2Wakorintho 9:7
TAFAKARI:Kwa mfano katika kutoa sadaka, kama tunavyoamini kutoa ni moyo, kwa hiyo Mungu akikutana na moyo wako anaangalia Imani uliyo nayo. Haijalishi umekuja na sadaka kiasi gani bali anaangalia imani yako ya utoaji.
SALA: Mungu baba, ninakiri ya kwamba vyote vilivyopo duniani ni mali yako,ninakushukuru kwa maana umenipa moyo wa kukutolea sadaka. Naomba Bwana uuhidhirishe uwepo wako kwangu, pindi nitoapo sadaka nikutane na wewe. Katika jina la Yesu naomba na kushukuru, Amen.

 

No comments:

Post a Comment