TAFAKARI: Kuna wakati mtu unaona muda
huu ni mdogo hautoshi kwa Mungu kuniskia pale nitakaposali, lakini kwa imani
ukipaza sauti na kuomba kwa nguvu, hatimaye maombi yako hujibiwa. Ni imani tu
inapeleka mtu kupata hitaji lake toka kwa Bwana ama kupona.
SALA: Bwana Mungu, tusamehe pale
ambapo tumekosa na kushindwa kukuamini wewe ya kuwa unatenda miujiza. Tusaidie
tuone na kwa imani tu tuwezeshe tuone zaidi na zaidi rehema zako za ajabu.
Katika jina la Yesu, tunaomba na kupokea, Amen. Karibuni katika blog hii, mahali ambapo utajifunza kuishi na kuenenda katika njia ya Kikristo na kusaidiana kukua kiroho kwa kusoma na kufundishana neno la Mungu. Ni matumaini yangu kwamba kila mmoja wenu atabarikiwa.
Tuesday, February 26, 2013
Neno la leo
Mt 9: 27 “Yesu alipokuwa akipita
kutoka huko, vipofu wawili wakamfuata wakipaza sauti, wakisema, Uturehemu mwana
wa Daudi”
Monday, February 25, 2013
Neno la leo
Mt 19: 21 “Yesu akamwambia, ukitaka
kuwa mkamilifu, enenda ukauze ulivyo navyo, uwape maskini nawe utakuwa na
hazina mbinguni; kasha njoo unifuate”
TAFAKARI: Katika hili zawadi ya bure
ya Mungu inakuja na gharama na ulazima. Ni juu ya sisi kutambua ni vitu gani
tunavijali zaidi. Lakini vilevile, tunapata faida kubwa pale tujuapo mualiko wa
Mungu ni wa haraka mno na kujua maisha ya kumfuata yeye ni ya utajiri mkubwa.
SALA: Bwana, tunaomba utangulize
matakwa ya maskini na wahitaji wako juu yetu hasa pale tunapokuwa na nafasi ya
kuchagua katika vile ulivyotupa. Katika jina la Yesu tunaomba na kupokea, Amen.Friday, February 22, 2013
Neno la leo
Mt 9:9 “Naye Yesu alipokuwa akipita
kutoka huko aliona mtu ameketi forodhani, aitwaye Mathayo, akamwambia, Nifuate.
Akaondoka, akamfuata”
TAFAKARI: Pengine wakati ule wa
kipindi cha utozwaji wa ushuru wa hali ya juu na unyanyaswaji wa watu, ulimuingia
Mathayo na kuchoshwa nao. Huenda aliskia habari za Yesu aliyekuwa anahubiri
habari njema kuhusu ufalme wa mbinguni, alikuwa anaponya wengi na kuwavuta
karibu. Aliposkia tu sauti ya Yesu akimuita aliruka haraka na kumfuata. Je,
tunajifunza nini juu ya habari hii?
SALA: Bwana tunaomba uwe mwenye
uvumilivu nasi pale tunapojishauri kuitikia mualiko wako wa kukufuata.Tunaomba
utuvute karibu nawe nasi tuwe miongoni mwa wafuasi wako, katika jina la Yesu
tunaomba na kupokea, Amen.Thursday, February 21, 2013
Neno la leo
Mt 8: 22 “Lakini Yesu akamwambia,
Nifuate; waache wafu wazike wafu wao”
TAFAKARI: Katika hadithi hii kitu cha
kwanza tunachotakiwa kufanya ni kuskia sauti ya Mungu na kufwata yale
anayotuelekeza, na mengine yatakuja baadae. Si rahisi kufanya hili kama
hujajitoa na huna hofu ya Mungu.
SALA: Bwana Mungu, tuwezeshe na utupe sikio la kusikia
ili tufuate sauti yako ya upendo pindi pale unapotuamuru kufanya kazi yako, kukufuata na kutupa maagizo ya kukutumikia wewe. Katika
jina la Yesu tunaomba na kushukuru, Amen. Wednesday, February 20, 2013
Neno la leo
Mt 8:19 “Mwandishi mmoja akamwendea,
akamwambia, Mwalimu, nitakufuata kokote uendako”
TAFAKARI: Ukisoma hadithi ya mwandishi
aliyeonekana katika kitabu hichi cha Mathayo kwa haraka unaweza kusema
ameonyesha maana ya kumfuata Yesu na Kujitoa kwa ajili yake (to follow and then
made a daring commitment). Lakini vilevile, waweza kusema kuwa alikubali
kumfuata bila kujua kuna gharama yake, yaani safari ya kwenda mbinguni sio
rahisi lazima mtu utakumbana na vikwazo. Mungu anahitaji watu ambao watajitoa
kwake kwa moyo wote na sio kwa kusita sita na kurudi nyuma.
SALA: Mwenyezi Mungu, tunaomba
utusaidie tuweze kusikia sauti yako na kuyatoa maisha yetu kwako ili tuishi kwa
kukutegemea wewe daima. Katika jina la Yesu tunaomba na kupokea, Amen.Tuesday, February 19, 2013
Neno la leo
Yohana 14:27 “Amani nawaachieni; amani
yangu nawapa; niwapavyo mimi sivyo kama ulimwengu utoavyo”
TAFAKARI: Mungu ametuachia amani. Na
vitu anavyotupa haviwezi kufanana na vile atoavyo mwanadamu. Yamkini ni magari
ya kifahari, pesa nyingi, na vingine vifananavyo na hivyo, kamwe haviwezi
kufanana na vitu atupavyo Mungu.
SALA: Mwenyezi Mungu tunakushukuru
kwa upendo wako wa ajabu. Umetupa amani katika nchi zetu lakini kwa kukosa
maarifa tumeshindwa kutumia ipasavyo yale unayotupa. Tusamehe Bwana na tunaomba
ukalete amani na upendo miongoni mwetu. Katika jina la Yesu tunaomba na
kupokea, Amen.Monday, February 18, 2013
Neno la leo
Zab 55:22 “Umtwike Bwana mzigo wako
naye atakutegemea, Hatamwacha mwenye haki aondoshwe milele”
TAFAKARI: Ukuu wa Mungu ni mkubwa
sana, hakuna chochote kitakachoweza kufananishwa naye.Mueleze shida zako naye
atakutendea mema.
SALA: Mungu wangu na Baba yangu, nashindwa kuelezea ukuu wako kwa jinsi ulivyo mkubwa. Maisha yangu
yamebadilika kutokana na matendo ya ajabu uliyonifanyia. Wewe mwenye haki
nitakushukuru siku zote za maisha yangu na najiachia kwako daima. Naomba na
kupokea katika jina la Yesu, Amen.
Subscribe to:
Posts (Atom)